Dodoma. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Taifa, Rais Jakaya Kikwete amewataka wanachama wa chama hicho kuacha unyonge na kusema uvumilivu una kikomo chake.
Aliyasema
hayo jana wakati anafungua kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) ya CCM,
kilicholenga kuweka msimamo wa chama kuhusu Rasimu ya Katiba Mpya ambayo
inaanza kujadiliwa Jumanne wiki ijayo.
“Tuna
uchaguzi mdogo, Iringa, Kalenga, tumeshapata mgombea na tumefanya hiyo kazi kwa
niaba yenu kwa sababu hatukupata muda wa kuitisha Kikao cha Halmashauri Kuu,
lakini mmetupatia mamlaka ya kufanya hivyo na Katiba imetupa fursa ya kufanya
uteuzi kwa niaba yenu,”alisema.
CCM
imemteua Godfrey Mgimwa ambaye ni mtoto wa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo,
marehemu Dk William Mgimwa, kupeperusha bendera katika uchaguzi mdogo
utakaofanyika baadaye mwaka huu. Dk Mgimwa hadi anafariki dunia alikuwa Waziri
wa Fedha.
Uchaguzi
mdogo wa ubunge Jimbo la Kalenga lililopo mkoani Dodoma. Mwenyekiti wa
Chama Cha Mapinduzi Taifa, Rais Jakaya Kikwete amewataka wanachama wa chama
hicho kuacha unyonge na kusema uvumilivu una kikomo chake.
Aliyasema
hayo jana wakati anafungua kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) ya CCM,
kilicholenga kuweka msimamo wa chama kuhusu Rasimu ya Katiba Mpya ambayo
inaanza kujadiliwa Jumanne wiki ijayo.
“Tuna
uchaguzi mdogo, Iringa, Kalenga, tumeshapata mgombea na tumefanya hiyo kazi kwa
niaba yenu kwa sababu hatukupata muda wa kuitisha Kikao cha Halmashauri Kuu,
lakini mmetupatia mamlaka ya kufanya hivyo na Katiba imetupa fursa ya kufanya
uteuzi kwa niaba yenu,”alisema.
CCM
imemteua Godfrey Mgimwa ambaye ni mtoto wa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo,
marehemu Dk William Mgimwa, kupeperusha bendera katika uchaguzi mdogo
utakaofanyika baadaye mwaka huu. Dk Mgimwa hadi anafariki dunia alikuwa Waziri
wa Fedha.
Uchaguzi mdogo
wa ubunge Jimbo la Kalenga lililopo mkoani
“Mpaka
sasa kwa dalili tulizonazo hatuna mgawanyiko wala hakuna misukosuko maana lile
la Arumeru (uchaguzi mdogo katika Jimbo la Arumeru Mashariki) lilikuwa na
misukosuko tangu tumeanza hadi tumemaliza,” alisema.
Katika
uchaguzi huo, uliofanyika Aprili mosi, 2012 mgombea wa Chadema, Joshua Nassari
aliibuka mshindi baada ya kumshinda Sioi Sumari wa CCM ambaye ni mtoto wa
marehemu Jeremiah Sumari, aliyewahi kuwa Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi mwaka
2008 hadi 2010.
Alitumia
fursa hiyo kuwapongeza viongozi na wanachama wa CCM katika kata 23, ambazo CCM
iliibuka na ushindi na kuwataka kuweka nguvu zaidi katika kuzikomboa kata nne
zilizoangukia mikononi mwa wapinzani.
Kata
ambazo wapinzani walishinda ni Sombetini (Arusha Mjini), Kiboroloni (Moshi
Mjini), (Njombe Mjini),zote zilichukuliwa na Chadema. Kilelema mkoani Kigoma
(NCCR Mageuzi).
Aidha,
Rais Kikwete alisema awali wakati wanaahirisha kikao cha Nec kilichopita,
walikubaliana watakuwa wakihamia mikoani kufanya vikao hivyo ambapo Mbeya
waliomba kuwa wenyeji na walikubaliwa.
Hata
hivyo, alisema waliamua kufanya tena kikao hicho mjini hapa, kwa sababu ya
agenda watakazozizungumza kwenye kikao hicho ambazo ni suala linalohusu
mchakato wa Katiba Mpya.
“Ili
tutakapoyamaliza, tujue tuweke misimamo gani itakayokwenda kwenye Bunge la
Katiba. Haina maana kuwa ile agenda yetu ya Mbeya tumeifuta, ahadi iko
palepale, kikao kitakachofuata cha kawaida kitafanyikia Mbeya,”alisema.
Awali Katibu
Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akimkaribisha Rais Kikwete, alisema kuwa
wajumbe wa Nec ni 372, lakini waliohudhuria walikuwa ni 368 (sawa na asilimia
98.3) hadi kikao kinafunguliwa.
source mwananchi
0 comments:
Post a Comment