
Bila kuwesti taimu, tudei ngoja nikusanue na stori moko ambayo naona kama ikiendelea tutazidi kulosti wana wakiwa na eji ndogo aiseee chaliiangu.
Unajua hili laifu halitaki kumbwela makachaa. Linataka ugangamale kiukweli kabisa. Longi taimu kitambo washkaji zangu walikuwa wanawasarendea mabaamedi kwamba baadhi yao ni makiksi yaani wanadili na bizinesi fekolo ya kuuza bodi kwa masela.
Tudei situwesheni imechenji. Mamaza walioko kwenye merieji wanaishi kwa hofu kinoma mazee. Wanagwaya kukwapuliwa mahazibandi zao na vichenchede wanaotupia nusu utupu kweye babashopu kisha kutoa sevisi kwa mahazibandi zao.
Oya acha kuzubaa mambo sasa hivi yapo saluni za mameni wewe. Tudei nakupa kitu ambayo sijatonywa wazazi nimeshuhudia mimi aloni. Nikiwa kaka mhariri masti nikemee michongo ambayo siyo mizuri kwenye sosayati.
Kwa makachaa najua mnanyaka ishu za masaluni ya mameni. Ebana kaka Kima babashopu za siku hizi siyo kukati nywele peke yake.
Sanuka wewe. Kukata nywele freshi bati kuna huduma nyingine. Inaweza kukuchukua kama wani hawa au zaidi kupata sevisi nyingine kama skrabu, manikiwa, pedikiwa, masaji na mipango mingine kama hiyo.
Oya masela hiyo ni geresha tu, ni chambo ya kukunasa kilainiii…Wakati unapewa huduma kaa hiyo, kuna meseji nyingine inakuwa delivadi kwako kuwa kuna huduma nyingine.
Ndiyo. Anachokifanya shori anayekufanyia moja ya sevisi tajwa hapo juu, anahakikisha anagusa sehemu zenye kimuhemuhe ili uzuzuke dheni utake mambo f’lani.
Mambo gani? Tulia wewe, hapa namaanisha mambo ya makopakopa. Kama ulikuwa hujui ngoja nikusanue. Ile ni bizinesi kama bizinesi nyingine bati bizinesi haramu au fekelo.
Iko hivi, kama shori akikufanyia hivyo na wewe ukazuzuka dheni ukabendi ukataka wepesi basi ujue unaua bendi laivu kozi uko shuwa kiasi gani kwamba demu yupo salama?
Unajua wakati ukipewa huduma hawawezi kuepuka kugusa wateja wao sehemu yenye hisia.
Kwa mfano wakati wa kufanya skarabu utakuta shori anaingiza vidole masikioni na kutekenya kwa makusudi kuona gari kama litawaka au la. Wakishajua wamewapagawisha wana kinachofuata ni kugawa namba ya foni kisha kuweka apointimenti na kwenda kugaragaza amri ya saba.
Samu taimu hao mashori huwa wanavuta mkwanja wa ziada kwa kisingizio cha kuthamini huduma waliyotoa kuwa ni klaski. Wenyewe wanaita tipu. Wazee wa tipu mpo? Ninyi endeleeni kutoa tipu mkiishi nyumba za kupanga mtajenga uzeeni. Yeleuuuwiii…Teeh…teeh…mbavu zangu miyeee…hahahaaa!
Kama hamuamini muulizeni mwanangu Hammy kilichompata kwenye saluni moko pale Kino. Duh! Jamaa kafanyiwa mambo hadi katoka nduki na maskrabu yake usoni eti anakimbilia homu akanawe! Chezea mashoro wa saluni? Itakula kwako daadeki!
src
GPL
0 comments:
Post a Comment