Inakuwaje watu wangu wa nguvu? Niaje…niaje kitaa hiyo? Hapo Roki Siti mzuka? Hapa vumbi tu! Ama nini? Kama vipi karibu jamvini tukisanue tugedha! Kwani kuna mbaya? Haina kwikwi jamaa yangu. Hapa mdogomdogo bati weka mbali na madongo…ooohooo! Utaambulia patupu ndani ya dakika ziro.
Kuna mnyama wangu mmoko kaniteli kuwa ni bora kupanga kwa faza hausi kuliko maza hausi! Unanyaka kwa nini? Selaa anakuteli kuwa washua hawana maneno kama mamaza. Hiyo ni kwa infomesheni yako tu. Tafakari!
Ebana eeeh! Lasti wikiendi arifu nilikuwa kitu cha Bwagamoyo. Dah! Kama unasikia pipo wanainjoi hili laifu, ibuka kitaa ile uone bata ndefu zinavyopigwa mazee hadi kuku wananuna. Kama una roho nyepesi uzalendo unaweza kukushinda na kujikuta ukitekeleza uhalifu utakaokozi upigwe nyuma ya nondo laifu lako lote lililorimeini.
Tudei ngoja tucheki na ishu moko hivi ambayo ipo siriazi dizaini f’lani bati naona kama wana wanaiteki simpo kinoma. Unajua ujana bana ni kitu ingine. Una chalenji zake kibwena na ili kukrosi seifu bila hatari inataka kuwa na roho ngumu kama wakata mkaa wenye hasira na maisha haya magumu.
Kwa wana wanaoperuzi sosho netiweki watakuwa wanainyaka freshi stori ya mbebiz mkare anakwenda kwa neimu la Betty. Kwa sasa tuseme R.I.P kwa Betty ambaye amededi juzikati. Aisee nilipoperuzi stori lake nilimaindi kinomanoma arifu.
Betty ni shori mkali kinoma na yupo biloo miaka 20. Ukicheki mafoto yake kwenye sosho netiweki utakubaliana na ishu ninayokwambia. Mtoto mzuri ile mbaya, alikuwa bado hajakomaa bati alikuwa veri femasi mitandaoni. Mei bii ni kwa sababu ya kupatikana onilaini muda mrefu kwa dei.
Kwenye hizi netweki yaani Instagram, Twitter, WhatsApp, Viber, Facebook, Skype na nyingine kibwena kuna hizi timu za kushambuliana.Mtoto mzuri kaingia kwenye mizinguo na timu moko ikaanza kumshambulia nini na nini, fulu kupeana stresi daadeki.
Fiyu hawaz kabla ya kuresti ini pisi, Betty alitukanwa na kukashifiwa kinoma na timu pinzani. Katika komenti zake Betty alionekana mwenye kukata tamaa kinoma kwa maana waliokuwa wakimtukana walimdhalilisha na inavyoonekana hakuwa na mtu wa kumshauri nje ya hizo sosho netiweki. Oya masela binadamu damu…bila damu sanamu!
Cheki hii situwesheni dheni tatua kitendawili hiki ambacho hata polisi kinawazingua kinoma.
Nini kimehapeni? Saa bee baada ya kuzinguana na wana kwenye sosho netiweki dheni mwili wake ukaokotwa tauni kwenye mtaro akiwa ameshavuta.
Dah! Sasa swali ni je, aliokuwa akizinguana nao ndo wamemdedisha au stresi za kukashifiwa ndo zimemsababisha akakata ringi au aliamua kujidedisha?Ndo kama hivyo, kama wewe ulikuwa unamtukana kwa mtandao unajisikiaje sasa sistaduu ameondoka?
Stori imetachi watu kibwena wanaotumia hizo sosho netiweki na matokeo yake ndo hayo. R.I.P Betty bati wengine mmepata lesoni?Hupigwi stopu kutumia hizo netiweki bati unazitumiaje? Kutupia mafoto ya ajabuajabu? Nooo! Itumie kuingiza mkwanja! Ama nini wana? Mmenisoma? Basi sii yuu wanangu!

0 comments:

Post a Comment

 
Top