BAADA ya kuandamwa sana katika mitandao ya kijamii kuhusu kutofunga vizuri vifungo vya suti yake,
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mhe. Stephen Wasira ameamua kumuona mbunifu wa mavazi wa kimataifa, Sheria Ngowi ili aanze kumtengenezea suti zake.
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mhe. Stephen Wasira ameamua kumuona mbunifu wa mavazi wa kimataifa, Sheria Ngowi ili aanze kumtengenezea suti zake.

Picha za Waziri Wasira zilienea mitandaoni alipopiga picha ya pamoja akiwa na Viongozi wa Kanisa la Kisabato kwenye Uwanja wa Taifa, Dar huku koti la suti yake likiwa limekosewa kufungwa vifungo.
Baadhi ya watumiaji wa mitandao ya kijamii walirusha picha mbalimbali zikimuonesha Mhe. Wasira huku mmoja wa watangazaji akisema kuwa iwapo akikubaliwa, atajitolea kuwa wabunifu wa suti zake za mitoko ili jambo hilo lisijitokeze tena.

0 comments:
Post a Comment