
Matokeo ya kidato cha nne
Siku moja baada ya Wizara ya Elimu, kutangaza Matokeo ya kidato cha nne na kuonyesha ufaulu kuongezeka kwa asilimia 15, wadau wa elimu wamepinga matokeo hayo kwa madai kuwa ubora wa elimu haukuangaliwa.
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Hatua hiyo inatokana na mabadiliko ya viwango vipya vya alama za ufaulu yaliyofanyika Oktoba mwaka jana, baada ya Serikali kuweka alama za kufaulu zisizobadilika katika daraja A mpaka F iliyotambuliwa kama kufaulu kusioridhisha.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM), Bashiru Ali alisema licha ya kiwango cha ufaulu kuongezeka, hakuna ubora wa elimu uliozingatiwa. Dk Ali alisema kinachochangia hali hiyo ni kuwapo kwa mfumo wa elimu wa kibaguzi, unaosababisha ubora wa elimu unashuka, kwa kuwa badala ya kupimwa kwa ujuzi na maarifa hupimwa kwa madaraja.
Mhadhiri ya Chuo Kikuu DUCE.
Dk Kitila Mkumbo wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Duce), alisema tatizo lililopo ni mfumo mbaya wa ufundishaji, badala ya kuwekeza nguvu kukuza taaluma, nguvu nyingi zimewekezwa kupanga madaraja.
Alisema matokeo hayo ni mazuri kwa Serikali, kutokana na kuzongwa na matokeo mabaya ya mwaka jana, lakini kitaaluma siyo mazuri (Matokeo ya kidato cha nne)
0 comments:
Post a Comment