
Kwani kuna tatizo? Hakuna tatizo!
Festi sharauti ziende kwa masela na washikaji zangu wote mlioibuka pale kati Uwanja wa Taifa kwenye Tamasha la Usiku wa Matumaini. Aisee siyo sekreti ilikuwa mzuksi hatare sana. Bata zilipigwa hadi kuku wakaona mawivu daadeki!
Bigi apu kwako mwenyewe kozi kufika kwako ndiyo mafanikio ya mpango mzima. Ama nini?
Afta sharauti turudi kwenye mastori moo. Aisee chaliiangu asikuchiti mtu.
Hapa unaondoa stresi kisha tabasamu pana kozi kuna wana mwaka unakatika bila tabasamu arifu. Ni fulu stresi deile mzazi.
Ebana kuna mwanangu mmoko anakwenda kwa neimu la Tom bati yeye humaindi kujiita Mr T hasa anapokuwa kitaani na washikaji. Mwana ana shori wake mkare aibu aisee.
Mtoto mzuri anaitwa G. Nikitaka kutumia spesi hii kumsifia G itachukua taimu kozi mbali na kuwa kifaa cha ukwehe, mama la mama ni waifu matirio. Yaani ni mama bora. Chezea kampeni ya mama na baba bora? Unaambiwa nawu deizi ni mwendo wa vipara so ukizubaa tu mafaza wanakubonyezea kitu yako!
Jamaa na shori wake ni wana kutoka hapo mji wa wagumu Moshi.
Si unajua zile za kusaka bingo baada ya kusota maskuli kitambo dheni ishu ni jinsi ya kufumania mkwanja?
Mshikaji ana braza’ke aliyemtangulia ambaye naye ana shori wake ambaye Mr T alikuwa hamjui. Kwa upande wake G naye ana sista’ke ambaye naye Mr T alikuwa hamnyaki.
Huku na huku Mr T na kifaa chake wakawa wanapanga dizaini ya kitu cha mereji nini na nini. Bifoo mshikaji wangu hajampeleka shori kwa homu, wani dei braza’ke alimteli kuwa anampeleka shori wake homu kileji so kama vipi watimbe kileji wote.
Mr T akaona isiwe kitu, akatimba kileji na mbuzi akaliwa kisusio flenga na kitu cha mbege kwa mbaaali. Kweli broo wake alimtambulisha mai waifu mtarajiwa dheni watu wakarudi tauni kuendelea na mbishe.
Wakati mzazi jembe akiwa kwenye mastori moo na shori wake yaani G akamwambia sista’ke anafunga kitu cha pingu za maisha so akamuomba kutoa kolabo ya kutosha. Kachaa wangu akamwambia sistaduu wake kuwa haina kwere kozi naye alimwambia broo wake ana ishu ka hiyo.
Deizi zikamuvu fasta kinoma. Shughuli zikazidi kupamba moto huku Mr T akihudhuria vikao vya preparesheni freshi. Lasti wikiendi ndo ilikuwa sendi ofu ya sista’ke G. Hapo ndo msala ulipotokea. Dah!
Mr T ambaye alikuwa amealikwa na shori wake alijikuta akipaniki baada ya kugundua kuwa broo wake alikuwa anamuoa sista’ke na shori wake wakati naye yupo kwenye mipango kama hiyo.
Mr T anakuteli kuwa yeye na G wamekuwa pamoko kwenye rilesheni kwa zaidi ya miaka saba. G naye kapaniki kinoma baada ya kugundua kuwa sista’ke anaolewa na broo wa mchumba’ke. Aisee noma sana!
Mmenisoma? Hebu jiweke kwenye pozisheni ya Mr T na G wake… mngechukua stepu gani kiroho safi kabisa.Kama huna ansa…sii yuu neksti wiki.
src
GPL
0 comments:
Post a Comment