
Taarifa
iliyotolewa hivi karibuni inayoonyesha kuwa deni la Taifa linakua kwa wastani
wa Sh2 trilioni kila mwaka, imepokewa tofauti, huku wengi wakilalamikia hali
hiyo.
Kulingana
na taarifa hizo za Serikali ya Tanzania ni kwamba mwaka 2005 Taifa lilikuwa na
deni la Sh10 trilioni, ambalo limekua hadi kufikia Sh27 trilioni mwishoni mwa
mwaka jana.
Kulingana
na hali ilivyo sasa, Tanzania inaelekea kupoteza sifa za kukopesheka; bado
asilimia 22 ya kufikia kikwazo cha kutopata mikopo.
Mikopo inatumikaje
Mbaya
zaidi hata mikopo hiyo imeonekana kutotumika kama ilivyotarajiwa.Katika
kudhihilisha hilo inaelezwa miaka ya 70, Serikali ilikopa Sh96 bilioni kwa
lengo la kuanzisha Kiwanda cha Viatu Morogoro, lakini kilifilisika.
Baada
ya kufilisika, kilibinafsishwa miaka ya 90, deni la fedha zilizotumika likawa
bado mzigo kwa wananchi wa Tanzania.
Waziri
wa Fedha, Saada Mkuya hata hivyo anajipa matumaini kuwa licha ya kuwa na deni
hilo, Serikali bado inayo nafasi ya kukopa fedha.
Kauli
hiyo inatokana na hatua ya Serikali kwa kushirikiana na taasisi za kimataifa
kufanya thathmini iliyokuwa na lengo la kuangalia uhimilivu wa deni hilo katika
kupata mikopo.
Tathmini
hiyo ya Septemba mwaka jana ilionyesha deni hilo linaweza kuhimili kwa sababu
viashiria vyote bado viko chini ya ukomo unaotakiwa.
Wachumi
wanasema kutokana na mazingira hayo, makadirio ya miaka kadhaa ijayo Serikali
inaweza kuingia kwenye kikwazo cha kupata mikopo endapo haitakuwa na mkakati wa
kulipa deni na kupunguza mikopo hiyo.
Profesa
Humphrey Mushi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) anasema kukopa siyo
dhambi lakini ni muhimu kuzingatia mikopo hiyo inatumikaje.
“Lazima
kujiuliza je, uwezo wa kulipa upo au la, siyo vizuri kukopa tu ili mradi; siyo
kukopa tu kwa sababu eti bado tunayo nafasi ya kuendelea kukopa,hiyo siyo
sahihi,” anasema Profesa Mushi na kuongeza;
Serikali
isijisahau katika mikopo hiyo kwa sababu eti tumepata ugunduzi wa gesi asilia,
ikumbukwe inaweza kukopa na gesi ikakosekana inakuwa ni hasara kubwa kwa taifa,
kwa hivyo ni muhimu kuwa makini na maeneo ya kuwekeza mikopo hiyo.
Tahadhari kwa Serikali
Akitoa
mifano, Profesa Mushi anasema kwa sasa Serikali inatakiwa kuhakikisha inatumia
fedha za mikopo katika miradi yenye tija katika uchumi wa Taifa.
“Serikali
ikope pale inapowezekana, siyo kukopa na kuwekeza katika mambo mengine yasiyo
ya maendeleo,” anasema.
Mbali
na hilo, Profesa Mushi anasema Serikali inatakiwa kuwa makini na taarifa za
wahisani juu ya mikopo.
“Wakisema eti
bado tuna vigezo vya kukopa tu haitasaidia, hao siyo wa kusikiliza sana, badala
yake iwe na utaratibu wa kutumia mawazo ya Watalaam wa ndani,” anasema
Wizara ya Fedha imejipangaje?
Mwandishi
wa makala haya alifanikiwa kufanya mahojiano na Waziri wa Fedha Saada Mkuya ili
kujua mikakati na tahadhali zilizopo katika wizara yake juu ya deni la Taifa.
Kwanza
kabisa Waziri Mkuya anasema mpaka sasa Serikali haijafikia uwezo wa kusitisha
ukopaji.
“Kulipunguza
deni hilo maana yake tusiendelee kukopa lakini sisi hatujafikia uwezo wa kuacha
kukopa kwa sababu mapato yetu ya ndani hayajitoshi,” anasema na kuongeza;
Tunachokifanya
kwa sasa ni kuhakikisha tunakuwa na utaratibu wa kupata mikopo itakayokuwa na
riba ndogo, yenye masharti nafuu.
Waziri Mkuya
anasema pamoja na kuendelea na ukopaji, wizara yake itakuwa makini na mikopo
hiyo katika mpangilio wa bajeti yake ikiwemo kupeleka fedha hizo katika miradi
ya maendeleo mbalimbali ya uchumi nchini.
Kila
mkopo tutakaochukua kwa sasa utaelekezwa katika miradi ya maendeleo hasa ile
inayochochea ukuaji wa uchumi na mapato ya ndani, kwa mfano miundombinu. Ni
kwamba siyo kila mradi utaombewa mkopo,” anasema Waziri Mkuya.
Pia
Serikali inaangalia njia nyingine za kukopa hapa nchini kupitia ushirikiano wa
pamoja kati ya sekta binafsi na umma (PPP).
“Zote
hizo ni jitihada za kuhakikisha tunapata mikopo inayokuwa na mabadiliko makubwa
ya uchumi wa taifa, pia itatusaidia kutofikia kwenye vikwazo vya kupata mikopo
kwa sababu uchumi unapokua hata kasi ya kufikia vikwazo inapungua,” anasema
waziri huyo.
Mazingira ya deni lenyewe
Mnamo
mwaka 2006, deni la Taifa lilikuwa asilimia 70 ya Pato la Taifa, ingawa msamaha
wa madeni ulipunguza kiwango hicho hadi asilimia 21 mwaka uliofuata.
Kwa
sasa deni hilo ni sawa na bajeti ya Serikali ya mwaka mmoja na nusu kwa mujibu
wa bajeti ya mwaka 2013/14 ya Sh17.7 trilioni. Kati fedha hizo, Sh20.23
trilioni zinatajwa kuwa ni deni la nje huku Sh6.81 trilioni deni la ndani Waziri
Mkuya anasema sababu za kuongezeka deni hilo ni pamoja na mikopo iliyopokelewa
na Serikali ambayo muda wake wa kulipa haujafika.
Aidha
malimbikizo ya deni la nje yanayofikia Dola 801.7 milioni kutoka kwa nchi
zisizo wanachama wa jumuiya ya wahisani, ni baadhi ya mambo yanayochangia kukua
kwa deni la Taifa.
Sourece
mwananchi
0 comments:
Post a Comment