Mwezi huu wa pili, ushasepa kudadaddeki, tunaelekea Machi, watu neksti wiki tutakuwa tunaongea ishu zingine. Wanangu wa mikoani kaeni fresh, blaza anaanza misele vere suni, tutakuwa tukipeana ratiba za hizi bata, uongo?

Enewei, mzuka upo wa kutosha?

Juzi kati nimezingua sana na mwanangu SogiDogi mitaa ya mbele, tukagundua kwamba tupo kwenye gemu longtaimu na mwisho wa siku ikaja nini ujue?

Sisi ni wazee, tukajiuliza kwa nini tusijiite Bakulutu?

Kuna kitu kikali kinakuja kuhusu watu wa longtaimu kwenye gemu, we kiskilizie, utainjoi mwanangu mwenyewe.

Wanangu mnaeondelea kusapoti Zee la Nyeti kwa miaka mingi nimerudisha ile aidia ya kuangusha mnuso wa miaka 16 ya kolam ya zee, kama ulikuwa unasoma miaka yote hii nicheki kwa kuingia kwenye peji ya Zee la Nyeti, inapatikana fesibuku

siku hizi, ukifika kule isake, halaf laiki!

Wiki hii nina ishu kama mbili hivi za kukupa, nimezipigia mzigo na kugundua kwamba kama ishu huiwezi ni bora kuwaachia wajuzi wa kazi hizo. Msele wa kwanza ulikuwa dauntauni, mitaa ya Posta mwanangu mwenyewe, nikakutana na bonge la kisanga, nilitumia mia tatu kwenye hii trip kwenda, kurudi nikala lifti ya Dj KU wa Times FM, sasa tauni nikakutana na ishu moja, kuna jamaa kaja kuchukuliwa maskani na wajomba, a.k.a polisi pale Bilikanas nje huku mtu mzima naangalia hivi.

Cha kushangaza ni nini ujue? Wakati wajomba wanamsomba mwana, washkaji zake wakawa kama hawana taimu hivi, wanamwangalia tu mchizi anaishia na mimi nilipoiona ile picha ikabidi nitulize kipago kwanza, waliposepa na mtu wao ndipo nikauliza, inakuwaje?

Nikapewa kwamba mwana wamemchoka ni mtu wa kupiga ishu mbovu kila mara na akipata mkwanja hawashirikishi wana, anaenda kula raha na mademu zake zikiisha anaibuka tena na siku akibambwa, wana ndiyo wanakomaa naye na mademu zake wanaingia mitini.

Umeona mwanangu? Mchizi miyeyusho, watu wamechoka, ishu  hizi unakula na wenzako, lakini wewe unakula mwenyewe?

Sio mjuzi! Dah, nikaona kweli kisha siku mbili tatu, tena kitaani kwangu unaambiwa, demu kaja jirani kwangu. So, unajua tena mwanao naishi karibu na mjumbe? Kaja kumshtaki mchizi wake kwamba kamwingizia demu ndani.

Umeelewa?

Yaani demu kaja kushtaki kwamba kaja kumtembelea mchizi wake, ndani kakuta kuna demu mwingine na yeye ndiyo kachuma na mchizi kila kitu, lakini haishi naye.

Mchizi akaitwa, mchizi kuja, ishu yenyewe ikamgeukia demu, kumbe demu hata wazazi wake hawapo tauni, anaishi mwenyewe lakini hakai na mchizi na hataki kupiga mbonji kwa mchizi eti mpaka ndoa.

Lakini akitoka kwa mchizi, baadaye unaweza ukasikia kaonekana disko na mchizi f’lani.

Demu hapiki, wala hafui, demu ye zake akija, anapiga mambo yetu yale, kisha anasepa, sasa mchizi kaivumilia miyeyusho mpaka kachoka, kaamua kuvuta kitu kipya.

Kuna ubaya mwanangu mwenyewe? Mi nikaona kama mchizi yuko sawa tu, mjumbe akashangaa nimeibuka na kuanza kumtemea shiti demu, wakati wanaendelea kushangaa, nikamchukua mchizi, nikampa bonge la hagi, kisha nikajisepea zangu mbele kwa mbele.

Mi mtu?

Mimi zee bwana
Mtu una boifrendi halaf unajifanya una shughuli zako, waache wanaojua kuhudumia wapige kazi, siku hizi kwanza mademu wengi kuliko mameni, sasa wewe ulileta miyeyusho watu wanamsomba na mchizi mwenyewe, wanakaa naye.

Hao ndiyo tunawaita wajuzi wa hizi kazi.

src

 mwanachi

 

 

0 comments:

Post a Comment

 
Top